Dialogue

Vocabulary

Learn New Words FAST with this Lesson’s Vocab Review List

Get this lesson’s key vocab, their translations and pronunciations. Sign up for your Free Lifetime Account Now and get 7 Days of Premium Access including this feature.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Notes

Unlock In-Depth Explanations & Exclusive Takeaways with Printable Lesson Notes

Unlock Lesson Notes and Transcripts for every single lesson. Sign Up for a Free Lifetime Account and Get 7 Days of Premium Access.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Transcript

Maadhimisho ya Mwaka Mpya Nchini Kenya
Tamasha ya mwaka mpya ni mojawapo ya sherehe ambazo husherehekewa kote ulimwenguni. Sherehe hii huja wiki moja tu baada ya sherehe ya Krismasi. Wakenya hawaachwi nyuma katika kuadhimisha sikukuu hii inayoashiria mwisho wa mwaka mmoja na mwanzo wa mwingine. Huwa ni wakati wa karamu na furaha watu wanapokutana na marafiki na jamaa zao. Watu hujawa na matarajio na kuweka maazimio yao kwa ajili ya mwaka mpya huku wakitumai ya kwamba mwaka mpya utaleta heri njema na fanaka katika maisha yao.Nchini Kenya, siku ya mwaka mpya huwa likizo na kwa hivyo wakati mzuri kwa familia na marafiki kukutana. Pia ni wakati ambapo watu kubadilishana zawadi na pia kutuma arafa za heri njema kwa marafiki na jamii. Wakenya wana njia mbalimbali za kuukaribisha mwaka mpya.Watu wengi hukutana katika makanisa, mijini na pia mashambani ili kumshukuru mungu kwa mwaka ulioisha na kuomba kuwa mwaka mpya uwe wa fanaka. Mwaka mpya hupokewa kwa shangwe na nderemo na baadaye umati husubiri waasi kutoka kwa wakleri. Wakristo husafiri kwa umbali kujiunga na wenzao kuukaribisha mwaka mpya kwa kuwa wanaamini hii ndiyo njia bora zaidi ya kuanza mwaka.Makundi mengine hasa vijana hukusanyika kwa tamasha na kuukaribisha mwaka mpya kwa mtindo. Wasanii mbalimbali hutumbuiza waliohudhuria. Mwaka mpya hukaribishwa kwa nyimbo na densi na vifaa vinavyolipuliwa hewani. Tamasha hizi hupangwa na mandhari ya kupitisha ujumbe fulani kuhusu masuala ambayo yanawaathiri.Wakenya wengine husherehekea kwa kwenda kujivijari katika sehemu mbalimbali za nchi. Nchi ya Kenya ina aina mbalimbali za ndege na wanyama ambao wamehifadhiwa katika mambuga mbalimbali; hivyo wakenya wana chaguo kubwa pa pahali watakakoenda. Kuna pia mwambao ambapo kuna fukwe na ziwa ambako wengi huenda kuogelea.Kuna pia kundi jingine ambalo hukutana katika vilabu kuukaribisha mwaka. Hapa vituko vya aina zote hufanyika , wengine hupanda juu ya magari huku wakipuliza vyombo kama 'vuvuzela' na kupiga kelele za shangwe.Raisi wa jamhuri hii pia hutarajiwa kutoa ujumbe wa mwaka mpya na kuwatakia wakenya mwaka wa fanaka.

Comments

Hide