Dialogue

Vocabulary

Learn New Words FAST with this Lesson’s Vocab Review List

Get this lesson’s key vocab, their translations and pronunciations. Sign up for your Free Lifetime Account Now and get 7 Days of Premium Access including this feature.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Notes

Unlock In-Depth Explanations & Exclusive Takeaways with Printable Lesson Notes

Unlock Lesson Notes and Transcripts for every single lesson. Sign Up for a Free Lifetime Account and Get 7 Days of Premium Access.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Transcript

UVUKO WA DARAJA
Mwangi Gicheru ni mwandishi wa kitabu hiki ambacho kina wahusika wa kuu watatu ambao ni; Karolina, Chuma na Kihuthu.
Kihuthu ni babake Karolina.
Chuma ni msimulizi na mfanyikazi wa familia ya Kihuthu.
Kihuthu ni tajiri wa kupindukia.
Karolina alianza mapenzi na Chuma, lakini jua kwamba wazazi wake hawangemruhusu aolewe na Chuma kwa ajili hali yake ya kijamii ilikuwa ya chini.
Karolina alishika mimba ya Chuma, jambo lililowaaibisha familia yake.
Chuma alijihurumia kwa ajili ya hali yake na wakati mwingine kujiona kama takataka ya kiwanda.
Alidhani kwamba Mungu alimuumba baada ya chakula cha mchana kwa kutumia mabaki ya viumbe.
Alidhani kwamba fedha ingeweza kumnunulia chochote.
Alidhani kwamba babake Karolina hangekuwa na tatizo naye kama angelikuwa na fedha.
Chuma alijuta kukutana na Kihuthu kwani aliona kama hili jambo lilimletea taabu.
Hivyo basi akaanza kujihushisha na wizi ili kumfurahisha Karolina.
Kwa bahati mbaya alipatika na akafungwa jela.
Karolina alitorokea kijijini ambako maisha yalikuwa magumu.
Baada ya kushikwa kwa Chuma, aliamua kurudi kwa familia yake.
Jelani, Chuma alikutana na Kisinga ambaye alimwingiza katika ujangili baada ya muhula wao jelani.
Chuma alienda Mombasa kumtafuta Karolina na kule kumwibia mtalii.
Kisinga alikamatwa na kufungwa jela tena.
Baadaye, Chuma alimpata Karolina ambaye alijaribu kumkimbia.
Alianguka kwenye gazi, kitendo kilichofanya Chuma ashtakiwe kwa jaribio la wizi na uaji.
Je, Chuma atafanikiwa kulivuka daraja la umaskini hadi utajiri? Mwangi Gicheru anaelezea maisha ya Chuma kwa kuchanganya upendo, furaha na utajiri.

Comments

Hide