Dialogue

Vocabulary

Learn New Words FAST with this Lesson’s Vocab Review List

Get this lesson’s key vocab, their translations and pronunciations. Sign up for your Free Lifetime Account Now and get 7 Days of Premium Access including this feature.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Notes

Unlock In-Depth Explanations & Exclusive Takeaways with Printable Lesson Notes

Unlock Lesson Notes and Transcripts for every single lesson. Sign Up for a Free Lifetime Account and Get 7 Days of Premium Access.

Or sign up using Facebook
Already a Member?

Lesson Transcript

Ken wa Maria
Ken wa Maria anafanya muziki wake katika lugha ya kikamba.
kwa sasa yeye ndiye msanii mmaarufu kutoka eneo la ukambani.
Nyimbo zake ni za mtindo wa 'benga'.
Ken anaalbamu kadhaa na zote kwa lugha ya kikamba.
Chakushangaza ni kuwa nyimbo zake zinaumaarufu kwa watu wa maeneo yote nchini hata wasioelewa kikamba.
Majina yake kamili ni Ken Wambua Nguze.
Yeye anapenda kujitambulisha kama mfalme wa nyimbo za kikamba na kila mmoja aliyehudhuria tamasha zake unauhakika wa jambo hili.
Ken huongoza bendi maarufu inayojulikana kama 'Yatta Orchestra International Band.'
Tofauti na wanamuziki wengi waofanya muziki pekee, Ken ni mwanasiasa na mjasiriamali anayehusika hasa na nyumba za kukodisha.
Kama mjasiriamali, Ken amelipa shilingi milioni 3 kwa nyumba katika sehemu ya Doonholm, Nairobi; anamiliki maduka matatu ya nguo mjini , pia ni mshirika katika Kinga Motors Umoja, kampuni inayohusika na magari yaliyotumika.
Yeye ni mmojawapo ya watu wanaomiliki kampuni ya Sunset Safaris - Pur jijini Mombasa.
Azimio la Ken wa Maria kuwania kiti cha ubunge lilikatika alipopokea vitisho vya kuuliwa kutoka kwa wanaodhaniwa kuwa wapinzani wake.
Hivyo basi, aliamua kumuunga mkono kiongozi wake katika siasa mheshimiwa Kalonzo Musyoka aliyekuwa mgombea mwenza Mheshimiwa Raila Odinga ambaye ni kiongozi wa chama cha muungano wa CORD.
Ken ambaye sasa anaumri wa miaka 36 ana mke na watoto wawili.
Licha ya muziki wake kupata soko kubwa mandarini, Ken hajawai onekana katika vyombo vya habari wala kujulikana kama mwana mziki aliyesifika sana lakini mambo haya hayamtishi moyo.
Katika mwaka wa 2001 Ken aliteuliwa kama mmoja wa waliokuwa wakigombea taji la East Africa Music Awards katika jamii ya nyimbo za mtindo wa kilingala.
Kulingana na yeye kuteuliwa kwake ni jambo la kutosha la kuonyesha kuwa muziki wake unafanya vizuri hata kama hajaweza kupata tuzo hilo.

Comments

Hide