| KUOKOLEWA KWA HELIKOPTA | 
                                                                
                                                                            | Kitabu hiki kimeandikwa na K W Wamitila aliyezaliwa tarehe 13 Juni mwaka wa 1965. | 
                                                                
                                                                            | Yeye ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Nairobi. | 
                                                                
                                                                            | Hii ni hadithi inayohusu kituko kizuri ambacho baadae kilienda mrama. | 
                                                                
                                                                            | Katika kitabu hiki, Zeke, kijana wa umri wa miaka kumi amshawishi Kate, binamu yake aliyekuja kumtembelea, ya kuwa andamane naye hadi kisiwa kilichokuwa hapo karibu. | 
                                                                
                                                                            | Wawili hawa waliondoka na kwenda kwa kile kisiwa bila kumfahamisha yeyote. | 
                                                                
                                                                            | Dalili ya mvua ilikuwa wazi hapo tu walipowasili ziwani. | 
                                                                
                                                                            | Zeke anaenda mbele na kumkaribia mvuvi mmoja anayemwomba awapeleke kisiwani bila malipo. | 
                                                                
                                                                            | Kwa mara ya kwanza, mvuvi anasita kuwapeleka kwa vile anahisi kuwa kuendesha mashua katika hali ile mbaya ya anga ingekuwa ni hatari lakini anabadili mawazo yake Zeke alipozidi kusisitiza. | 
                                                                
                                                                            | Mvuvi anawapeleka Zeke na Kate kwenye kisiwa na kurudi kuvuvi kwa haraka baada ya kuwafikisha pale kisiwani. | 
                                                                
                                                                            | Peke yao, vijana hawa wawili wanaanza kuvumbua kisiwa hiki ambapo wanafanikiwa kupata pango lililo kuwa ndani ya mbuyu uliofaraghiwa. | 
                                                                
                                                                            | Waliamua kuingia ndani zaidi ya ile pango ambamo walibebeka na mazuri yaliyokuwa ndani. | 
                                                                
                                                                            | Kulikuwemo maandishi ya kigeni, alama za kusisimua kwenye kuta na mawe meusi zilizofanya akili za vijana hawa kuduwaa na kubebeka zaidi. | 
                                                                
                                                                            | Mvua ulianza kunyesha kwa uzito na mvuvi akaondoka kwa haraka na kusahau kuwachukua vijana hawa. | 
                                                                
                                                                            | Alikumbuka kuhusu vijana hawa mara tu alipofika ukingoni. | 
                                                                
                                                                            | Kurudi katika kile kisiwa ili kuwaokoa Zeke na Kate ilikuwa haiwezekani kwa vile mvua ulivyokuwa ukinyesha kwa wingi, ndivyo hali ya hatari ilivyoendelea kuzidi. | 
                                                                
                                                                            | Ngazi ya maji katika ziwa iliendelea kupanda na wakati huu kisiwa nacho kilikuwa kinatokomea haraka na maji yalikuwa yameanza kuingia katika ile pango. | 
                                                                
                                                                            | Vijana hawa watajitoaje katika mkasa huu? Isitoshe, wazazi wa vijana hawa hawana habari kuhusu kilicho wapata wanao. | 
                                                        
                     
Comments
Hide